SANAA YA LUGHA

POEMS, STORIES, COMMENTS, NA KADHALIKA

MWENYE MATUSI

Posted by Tabu Bin Tabu on November 10, 2011

Yako majina ya vitu, mengine yasiyotajwa,

Yashangaza kuna watu, wenye uovu kujawa,

Waona kuwa si kitu, ni kama wanaolipwa,

Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.

 

Mtu sio hayawani, anatumia akili,

Kuboboka hadharani, huwa ni kwake katili,

Matusi siwe kinywani, kama lusu tafadhali,

Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.

 

Mdomo wako ni moto, wewe mja nakwambiya,

Wanena mambo mazito, hutaki kuyawaziya,

Ulimi wako ufito, mwilini wateketeya,

Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.

 

Katu hutokaa tuli, kwa kweli tumefahamu,

Wewe ni ndumakuwili, mdomo wako ni sumu,

Wafitini kwa ukali, na kuua kama pumu,

Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.

 

Hauna wakati wako, na kazi kwako hauna,

Kinywani hauna mwiko, mpyaro unajivuna,

Pasipo masikitiko, sokoni hutukanana,

Thawabu yako motoni, sikua mwenye matusi.

 

Utamkacho laana, ulimi wako huchungi,

Na lusifa wafanana, u kama mvuta bangi,

Unaitana majina, visivyotajwa kwa wingi,

Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.

 

© Tabu Bin Tabu

24-10-2011

Advertisement

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out / Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out / Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out / Change )

Connecting to %s

 
Follow

Get every new post delivered to your Inbox.